Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limetangaza leo Mei 27, 2016 kuanza kwa mchakato wa kuchukua fomu za kugombea uongozi katika Klabu ya Young Africans ya Dar es Salaam inayotarajia kufanya uchaguzi tarehe 25 Juni mwaka huu.
Nafasi zinazogombewa ni pamoja na nafasi ya Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na wajumbe wanane wa Kamati ya Utendaji.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi, Aloyce Komba fomu zinapatikana katika ofisi za TFF zilizoko Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Ilala jijini Dar es Salaam. Mwisho wa kuchukua fomu ni tarehe 31 Mei, 2016.
Mashabiki wa timu ya yangawww.mashagmg.blogspot.com
Axact

MASHA GMG

Asante kwa kutembelea www.mashagmg.blogspot.com, endelea kuhabarika zaidi kila siku kwa kupata habari,Michezo,Burudani, Music na Video mbalimbali.

Post A Comment: